Fizimedia: Achomwa moto kwa jili ya wizi
Écrit par FiziMediaCongo sur juillet 19, 2019

_Leo tarehe 19/07/2019,usiku wamanane raia wenye asira kali walimpiga na kumchoma kijana ambaye hata sasa hajajulikana ni wakabila gani huko; ni huko wilayani fizi tarafani ngandja ndani ya kijiji cha misisi_.
_Raia hao waliojichukulia sheria mkononi walikwenda kuripotia polisi huku wakionyesha vitu walivyo mshika navyo ambavyo ni begi ya nguo na begi ya bangi_.
_Vyombo vya sheria(polisi),waliwaweka chini ya ulinzi wale walio jitokeza kuripotia tukio hilo huku wakiwa na bagi hizo walizo mkuta nazo mwalifu huyo_.
_Ikumbushwe kwamba vitendo vya wizi na ujambazi wakutumia silaha hata kuua mwenye mali kijijini misisi vyaimbwa kama wimbo wataifa,mbaya zaidi raia wanapo washika watuhumiwa na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria hamna atuwa yoyote muhimu inayo chukuliwa na vyombo husika, ndio sababu ya raia kuchukuwa jukumu yakujishikia sheria mkononi pale wanapo shika mtuhumiwa._
_by: Nondo wa mukalay ._
_chanzo:mkaaji wa misisi_
fizimedia.com
Copy right© fizimedia.com